Subscribe:

Ads 468x60px

Labels

FREEMASONS ni jamii ya siri (secret society)

FREEMASONS ni jamii ya siri (secret society) inayotisha duniani, njama zao za kuitawala dunia ifikapo Desemba 2012 ni tisa, kumi ni unyama wa kutisha waliomfanyia aliyekuwa Kiongozi wa Libya, Muammar Gaddafi.

Memba wa Freemasons hususan wale wanaomuabudu Shetani, Lucifer (Jini Mkuu), wanadaiwa kumchana Gaddafi kifuani, wakaikinga damu yake na kuihifadhi kwenye glasi kabla ya kuitumia katika kafara nzito.
Mtandao mmoja wa kidini umeandika kuwa damu ya Gaddafi, ilichanganywa na ya mbuzi aliyechinjwa ili kutolewa kafara katika kuadhimisha kukamatwa, kuteswa na hatimaye kuuawa kwa Gaddafi.

Katika habari hiyo, ilielezwa kuwa Freemasons walichukua kiasi kidogo cha damu ya Gaddafi na kuimimina kwenye ile ya mbuzi ambayo ndiyo ilikuwa nyingi na kuhifadhiwa kwenye chombo kimoja.

Habari zinafafanua kwamba baadhi ya Freemasons walikunywa, wengine walilamba na kunawa katika kusherehekea kuingiza mizizi yao ndani ya nchi yenye utajiri mkubwa wa mafuta (Libya).

Hata hivyo, kati ya wafuasi waliohudhuria kafara hiyo ni idadi ndogo mno waliokunywa damu ya Gaddafi iliyochanganywa na ya mbuzi, kwani wengi walilamba na kunawa, ikiwa ni ishara ya kutambua utukufu wa kiongozi wao, Lucifer.

“Damu iliwekwa kwenye glasi, aliyetaka kunywa, alimimina kidogo kwenye glasi ya peke yake, waliolamba waliingiza vidole na kulamba kisha wakanawa,” uliandika mtandao huo.

Kwa mujibu wa mitandao inayochambua mambo ya Freemasons, jamii hiyo ya siri hupenda damu ndiyo maana maadhimisho yao husindikizwa na kafara ya kuchinja wanyama hususan mbuzi.

Maalim Hassan Yahya Hussein ambaye ni mnajimu mwenye utaalamu mkubwa wa falsafa za Freemasons, naye alilithibitishia gazeti hili kuwa jamii hiyo hupenda damu kwa sababu humfurahisha kiongozi wao mkuu, Lucifer.

“Kuchinja na kuona damu kuna maana kubwa mno kwa Freemasons, wanapenda sana damu,” alisema Maalim Hassan.

NJAMA NI ILE ILE
Inaelezwa kuwa Freemasons ipo kwenye mkakati thabiti wa kuitawala dunia kabla ya Desemba 2012, hivyo imekuwa ikiratibu sera zake kwa kuangusha tawala za nchi mbalimbali ambazo viongozi wake wameshindwa kuendana na matakwa yake kama ilivyokuwa kwa Gaddafi.

Maalim Hassan aliliambia Uwazi: “Freemasons inapambana kutwaa mamlaka ya nchi tajiri kama Libya, inawaondosha viongozi ambao hawaendani na matakwa yao. Shabaha ya Freemasons pia ni kupambana na Uislam pamoja na Ukristo.

“Ipo wazi kuwa lengo lao ni kuitawala dunia, kwa hiyo wanasimamia kuona hilo linawezekana kwa kuhakikisha Uislam na Ukristo unaishiwa nguvu na Shetani anashinda hapa duniani,” alisema Maalim Hassan ambaye ni mrithi wa kazi za marehemu Sheikh Yahya.

Aliongeza: “Mkakati mkubwa zaidi ni kuhakikisha dunia inaabudu Dini ya Shetani, wanataka kila mtu awe chini ya mamlaka ya Jini Mkuu, Lucifer. Dunia nzima itawaliwe na serikali moja na iwe na sarafu moja.”

AFRIKA MASHARIKI YACHIMBWA
Kuangushwa kwa Gaddafi siyo suala la mzaha kwa Afrika, kwani inadaiwa kuwa Freemasons kupitia Jeshi la Kujihami la Nchi za Magharibi (Nato), inatekeleza sera zake kwa vitendo kwa nchi ambazo viongozi wake wameshindwa kukidhi matakwa yao.

Inaelezwa kuwa Freemasons hawapendi nchi kuungana na kubainisha kuwa ndiyo maana wameanza kuichimba Jumuiya ya Afrika Mashariki na ili kuidhoofisha, wameingiza agizo la kukubali ndoa za jinsi moja.

Habari zinasema kuwa Serikali ya Uingereza imekuwa ya kwanza kutumiwa na Freemasons katika kuhakikisha nchi zote zinazounda Jumuiya ya Madola zinapitisha sheria zinazokinzana na maandiko matakatifu yanayoaminiwa na waumini wa Dini za Kiislam na Kikristo.

Imeelezwa kuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki nguzo yake ni Tanzania, Kenya na Uganda ambazo ni wanachama wa Jumuiya ya Madola, hivyo agizo la ndoa za jinsi moja lengo lake ni kuzigawa kati ya zile zitakazokubali na zitakazokataa ili mwisho wake ziwe na mfarakano.

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino (Saut), Profesa Mwesiga Baregu, alizungumza kupitia runinga moja hivi karibuni kuwa anguko la Gaddafi Libya ni ishara mbaya kwa vyama vikongwe kama Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Alisema, nchi za magharibi hazipendi kuona vyama vikongwe vikishika madaraka kwa muda mrefu, kama ilivyo kwa CCM ambacho kinaongoza nchi tangu uhuru (Tanganyika mwaka 1961, Zanzibar 1964), kikiwa ni mtoto aliyezaliwa baada ya Tanu na ASP kuungana.

Angalizo hilo la Baregu, linatishia pia amani ya utawala wa Rais wa Uganda, Yoweri Museveni na chama chake cha National Resistance Movement (NRM), kwani yupo madarakani kwa miaka 25 sasa (alianza kutawala Januari 26, 1986).

Rais wa Kenya, Mwai Kibaki na chama chake cha People National Unit (PNU) ndiyo anapona kwenye angalizo hilo, kwani kuna mabadiliko makubwa ya vyama tawala nchini kwake, katika mihula miwili kati ya mwaka 2002 na 2012, tayari vimeshaongoza viwili. (Mwaka 2002 hadi 2007, chama tawala kilikuwa Narc).

VITA YA IMANI
Maandiko yanasema kuwa nyakati za mwisho kutakuwa na tishio la dunia kutawaliwa na Dini ya Shetani ambapo zama hizo zikifika kutakuwa na mfumo utakaozuia mtu yeyote kupata huduma za kijamii mpaka awe mwanachama na atatambulika kwa chapa 666.

Habari zaidi zinaeleza kuwa Freemasons wanatumia njia mbalimbali kuhakikisha ulimwengu mzima hakuna anayeamini dini za Mungu na wanapambana kuhakikisha hata Yesu (Nabii Isa) atakaporejea akute hakuna aliye tayari kukombolewa.

Katika kuhakikisha wanapambana na nguvu ya Yesu, Freemasons wamekuwa wakitumia damu ndiyo maana hutoa kafara kwa kuchinja wanyama hasa mbuzi au kondoo wenye pembe zinazotengeneza alama ya V kwa imani kwamba huwaongezea nguvu ya kuishika dunia.

0 comments:

Post a Comment

Asante kwa kusoma habari hii! Tafadhali acha tupia maoni yako HAPA!