Subscribe:

Ads 468x60px

Labels

Showing posts with label GALLERY. Show all posts
Showing posts with label GALLERY. Show all posts

Kuna wakati natamani sana... - DAVINA

“MOYO wangu umegandwa na mavumbi, macho yamepofuka kwa machozi, kwani mateso yangu hayapimiki kwa mizani, kila mtu ananihukumu kwa uongo na hadithi za kutunga juu ya ndoa yangu pasipo kujua ukweli,” ndivyo anavyoanza kusimulia staa wa filamu za Kibongo, Halima Yahya ‘Davina’ akielezea wakati mgumu anaokutana nao baada ya kuwepo na mgogoro kwenye ndoa yake.
Akizungumza kwa njia ya simu na mwandishi wetu hivi karibuni, msanii huyo alisema kila mahali anapopita ananyooshewa vidole kwa watu kumhukumu kuwa ni mkorofi kwenye ndoa yake jambo ambalo halina ukweli.
Akaeleza kuwa, siri za ndoa huzijua wahusika na kwamba hata yeye kufikia hatua ya kutengana na mumewe anajua chanzo ni nini na si rahisi kumueleza hata mama yake mzazi, ila watu wanatumia maneno makali yanayomuumiza.
“Kila mtu anasema analolijua, hakuna aliyenilazimisha kuolewa, kilichonifarakanisha na mume wangu tunakijua sisi wawili (yeye na mumewe), labda na watu wangu wa karibu, lakini kwa sasa maneno yamekuwa mengi sana, tena yenye kuumiza kiasi kwamba kuna wakati natamani hata kujitoa uhai.
“Vitu vingine ni vya ndani sana hata mama yangu mzazi siwezi kumwambia, ila maneno yamenizidia, haya, huyo Mike wanayemsema natoka naye, jamani nimemjua Mike kabla ya mume wangu, ilikuwaje nisitoke naye zamani ije kuwa leo? Naumia miye jamani, Mungu anajua, ipo siku kila kitu kitakuwa wazi,” alisema Davina kwa sauti ya uchungu.


Chanzo: Bongomovies

Wastara: Yusuph Mlela Anafanana Vitu Vingi na Sajuki

Staa wa Bongo Movies, Wastara Juma amefunguka na kumwagia sifa muigizaji mwenzake, Yusuph Mlela kuwa ni mtu ambaye anafanana vitu vingi na aliyekuwa mume wake, marehemu Sajuki  na kusisitiza kuwa huwa hachoki kufanya naye kazi.

Kupitia ukurasa wakekwenye mtandao wa instagram, Wastara aliweka picah hiyo hapo juu na kuandika;

Mama na mwana mama na baba nimeipenda kama ilivyo ila truelly huyu jamaa nampenda mfano hakuna mpole muelewa hana makuu anao ubinadaamu hana ugomvi na mtu mpole hajui kufoka wala kugombana akikasirika dakika 2 tu anarudi kuwa normal sichoki kufanya naye kazi namchukulia ni mdogo wangu wa tumbo moja namfananisha vitu vingi na Sajuki si mwingine this is Yusuph Mlela au Mlelandro

CHUCHU HANS NI WIFE MATERIAL - VINCENT KIGOSI (RAY)

Muigizaji mahiri wa kiume hapa Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray’amefichua siri iliyomfanya kunasa kwa staa mwenzake Chuchu Hans, na hata kupata msukumo wa kumuweka hadharani tofauti na tabia yake ya nyuma ya kutopenda kumuanika mpenzi wake.
Akizungumza na gazeti la Risasi akiwa kwenye tamasha la kimataifa la Filamu ‘ZIFF’ lililofanyika visiwani Zanzibar, Ray alisema kilichomsukuma kumuanika Chuchu ni mambo yake adimu ambayo huwezi kupata kwa mwanamke mwingine.
     Alisema anamuona kuwa na tabia zote za mke, ndiyo maana aliweza kumtambulisha kwa jamii kwa kuwa ana imani naye kwa kila kitu hivyo yuko huru watu kumfahamu.
        “Bwana huyu mwanamke ana vitu vyake adimu sana, na kwa kweli nampenda na ana chembechembe zote za kuwa mke ndiyo maana nilikuwa huru kumuweka wazi bila wasiwasi wowote,” alisema Ray ambaye pia aliwahi kutoka kimapenzi na Johari.

Chanzo:GPL